Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo matendo-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo matendo-ya-Mungu. Onyesha machapisho yote

Jumatano, 20 Februari 2019

Maneno ya Mungu | Ni Lazima Wale Wanaofaa Kukamilishwa Wapitie Usafishaji

Mwenyezi Mungu anasema:" Kama unamwamini Mungu, ni lazima umtii Mungu, uweke ukweli katika vitendo na utimize wajibu wako wote. Zaidi ya hayo, ni lazima uelewe mambo unayopaswa kupitia. Ikiwa unapitia tu kushughulikiwa, kufundishwa nidhamu na hukumu, kama wewe unaweza tu kumfurahia Mungu, lakini huwezi kuhisi wakati Mungu anakufundisha nidhamu au kukushughulikia, hili halikubaliki. Labda katika wakati huu wa usafishaji unaweza kushikilia msimamo wako. Hii bado haitoshi; ni lazima uendelee mbele.