Ijumaa, 17 Novemba 2017

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V Sehemu ya Kwanza

Kanisa la Mwenyezi Mungu,Umeme wa Mashariki
Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V

Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V Sehemu ya Kwanza

Utakatifu wa Mungu (II)

Mwenyezi Mungu alisema,Habari za jioni kila mtu! (Habari ya jioni Mwenyezi Mungu!) Leo, kaka na dada, hebu tuimbe wimbo. Tafuta mmoja ambao mnapenda na ambao mmeimba mara nyingi kabla. (Tungependa kuimba wimbo wa neno la Mungu “Upendo Safi Bila dosari.”)
Kiitikio: “Upendo” unarejelea hisia safi bila dosari, ambapo mnatumia mioyo yenu kupenda, kuhisi, na kuwa wa kufikiri. Katika upendo hakuna masharti, hakuna vizuizi, na hakuna umbali. Katika upendo hakuna tuhuma, hakuna udanganyifu, hakuna mpango, na hakuna ujanja. Katika upendo hakuna chaguo na hakuna chochote kichafu.
1. Iwapo mna upendo kama huo, basi hamdanganyi, hamlalamiki, hamsaliti, hamuasi, hamchukui, ama kuuliza kupokea chochote ama idadi fulani. Iwapo mnapenda, basi mnatoa kwa furaha.
2. Iwapo mna upendo kama huo, basi mnavumilia magumu, na kushirikiana na Mungu. Mnaweza kupeana vyote mlivyo navyo kwa sababu ya Mungu: familia zenu, siku zenu za baadaye, ujana wenu, na ndoa zenu. Vinginevyo, upendo wenu si upendo hata kidogo, lakini ni udanganyifu na usaliti!
Huu ulikuwa wimbo mzuri kuchagua. Mnapenda kuimba wimbo huu? (Ndiyo.) Mnahisi nini baada ya kuimba wimbo huu? Mnaweza kuhisi upendo wa aina hii ndani yenu? (Siyo vile bado.) Ni maneno gani kutoka ndani ya wimbo huu yanakugusa kwa kina? (Haya ni: Katika upendo hakuna masharti, hakuna vizuizi, na hakuna umbali. Katika upendo hakuna tuhuma, hakuna udanganyifu, hakuna mpango, na hakuna ujanja. Katika upendo hakuna chaguo na hakuna chochote kichafu. Lakini ndani yangu bado naona uchafu na pia naona wapi najaribu kufanya mipango na Mungu, maeneo niliyo na upungufu, kwa hivyo ninapofikiria kuhusu mimi leo kwa kweli sijafikia aina ya upendo ulio safi na bila dosari. ) Kama hujafikia aina ya upendo ambao ni safi na bila dosari, una upendo wa aina gani? Una kiwango kipi cha upendo ndani yako? (Niko tu katika hatua ambapo niko tayari kutafuta na nina hamu.) Kulingana na kimo chako mwenyewe na kutumia maneno yako mwenyewe kutoka kwa uzoefu wako mwenyewe, umefikia kiwango kipi? Je, una udanganyifu, una malalamiko? (Ndiyo.) Je, una madai ndani ya moyo wako, kuna vitu ambavyo unataka na kutamani kutoka kwa Mungu? (Ndiyo, kuna hivi vitu vilivyo na doa.) Vinajitokeza katika hali gani? (Wakati hali ambayo Mungu amenipangia hailingani na fikira zangu ya vile inapaswa kuwa, ama wakati matakwa yangu hayajatimizwa, nitaonyesha aina hii ya tabia potovu.) Nyinyi huimba wimbo huu mara nyingi? Mnaweza kujadili vile mnaelewa “upendo safi bila dosari”? Na mbona Mungu anafafanua upendo namna hii? (Naupenda wimbo huu sana mimi mwenyewe kwa sababu kwa kweli naweza kuona kwamba upendo huu ni upendo kamili. Hata hivyo, nahisi umbali kiasi na kiwango hicho. Sasa niko tu katika hatua ambapo niko tayari kutoa mambo fulani na kuvumilia baadhi ya gharama katika kufuatilia ukweli, lakini punde tu kitu kinaathiri siku zangu za usoni na kudura yangu, ninahisi kuchanganyikiwa ndani yangu. Naona kwamba ndani yangu nina imani kidogo kwa Mungu.) (Sasa nahisi kwamba bado niko mbali sana kufikia upendo wa kweli, lakini kuna baadhi ya maeneo ambapo nimeweza kuendelea mbele kuufikia, njia moja nafanya hivi ni kupitia nguvu ambayo maneno ya Mungu yananipatia na njia nyingine ni kwamba katika hali hizi nashiriki na Mungu kupitia maombi. Hata hivyo, inapohusiana maoni yangu ya uwepo, nahisi kwamba wakati mwingine siwezi kuyashinda.) Umewahi kufikiria kuhusu vitu ambavyo vinaweza kuwa vinakuzuia nyakati hizo huwezi kuyashinda? Umewahi kuchunguza maswala haya? (Ndiyo, nimekuwa nikichunguza na kwa sehemu kubwa ni kiburi changu na majivuno na pia matarajio yangu ya siku zangu za baadaye na kudura yangu ambavyo ni kizuizi kikubwa.) Wakati matarajio ya siku zako za baadaye na kudura ni kizuizi kikubwa, umewahi kufikiria kuhusu mbona ni kizuizi kikubwa? Ni vipi siku za baadaye na kudura vinaweza kuwa kizuizi? Unataka nini kutoka kwa siku zako za baadaye na kudura yako? (Siko wazi sana katika suala hili, wakati mwingine najipata katika hali ambapo nahisi sina siku za baadaye na kudura ama wakati mwingine nahisi hata kwamba sina hatima kwa kile ambacho Mungu amenifichulia. Katika nyakati hizi nahisi mnyonge sana na nahisi kwamba hii imekuwa kizuizi kikubwa kwa mimi mwenyewe. Hata hivyo, baada ya kipindi cha uzoefu na kupitia maombi, hali inaweza kugeuka, lakini bado nahisi mara nyingi kusumbuliwa na suala hili.) Unarejelea nini kwa kweli unaposema “siku za baadaye na kudura”? (Inamaanisha kwamba wakati Mungu amenipangia baadhi ya hali, nahisi kuwa mbali sana na mahitaji Yake. Wakati mwingine nastaajabu iwapo Mungu ananifichua ama la na nahisi kwamba sina kudura ama hatima, na nahisi mnyonge sana.) Mnarejelea nini mnaposema “siku za baadaye na kudura”? Kuna kitu mnachoweza kuashiria? Ni picha ama kitu mlichofikiria ama ni kitu mnaweza kweli kuona? Ni kitu halisi? (Ni hatima.) Hatima ni nini? Siku zako za baadaye ni nini? Katika kila mioyo yenu mnapaswa kufikiri, wasiwasi mlio nayo katika mioyo yenu kuhusu siku zenu za baadaye na kudura zenu inarejelea nini? (Ni kuokolewa na kusalimika, na matumaini ya kufaa polepole ili kutumiwa na Mungu na kutekeleza wajibu wangu hadi katika kiwango cha juu kupitia njia ya kufanya wajibu wangu. Vitu hivi mara nyingi vinafichuliwa na Mungu, na nahisi kwamba nina upungufu.) Kaka na dada wengine wanapaswa kujadili, unaelewaje “upendo safi bila dosari”? (Hakuna chochote kichafu kutoka kwa mtu binafsi na hadhibitiwi na siku zake za baadaye na kudura zao. Licha ya vile Mungu anamtunza, anaweza kutii kikamilifu kazi ya Mungu, na pia kutii mipango ya Mungu na kumfuata Yeye hadi mwisho kabisa. Upendo wa aina hii tu kwa Mungu ni upendo safi bila dosari. Ni wakati tu ninapojilinganisha na hilo ndipo ninapogundua kwamba katika miaka michache ambayo nimemwamini Mungu, nimeweza, juujuu, kutoa vitu fulani ama kuvumilia baadhi ya gharama, lakini sijawahi kuweza kweli kumpa Mungu moyo wangu. Wakati Mungu ananifichua, nahisi kana kwamba nimeainishwa kama mtu ambaye hawezi kuokolewa, na nakaa katika hali hizo hasi. Najiona nikifanya wajibu wangu, lakini wakati huo huo nikijaribu kutekeleza mipango na Mungu, na kutoweza kumpenda Mungu kwa moyo wangu wote, na kwamba hatima yangu, siku zangu za baadaye, na kudura yangu yote daima yako kwa akili yangu. Nakumbuka ushirika wa mwanadamu ulisema wakati mmoja kwamba tunapaswa kulipisha upendo wa Mungu kwa kutekeleza wajibu wetu, kwamba upendo lazima uonyeshwe kwa kweli, na sio tu maneno matupu. Kwa kulinganisha nahisi mbali sana na upendo huu.)
Inaonekana kwamba mmeimba wimbo huu mara nyingi na mna baadhi ya uelewa kuuhusu na kwamba kuna uhusiano fulani na uzoefu wako halisi. Hata hivyo, karibu kila mtu ana viwango tofauti vya kukubali kila kirai katika wimbo “Upendo Safi bila Dosari.” Watu wengine wako radhi, watu wengine wanatafuta kuweka kando siku zao za baadaye, watu wengine wanatafuta kuweka kando familia zao, watu wengine hawatafuti kupokea chochote. Bado wengine wanajihitaji kuwa bila udanganyifu, bila malalamiko, na kutoasi dhidi ya Mungu. Kwa nini Mungu angetaka kupendekeza aina hii ya upendo na kuhitaji kwamba watu wampende namna hii? Hii ni aina ya upendo ambao watu wanaweza kuufikia? Hiyo ni kusema, watu wanaweza kupenda namna hii? Watu wanaweza kuona kwamba hawawezi, kwa sababu hawamiliki kamwe upendo wa aina hii, na wakati hawaumiliki, na kimsingi hawajui kuhusu upendo, Mungu anazungumza maneno haya, ambayo ni mageni kwao. Kwa sababu watu wanaishi katika dunia hii, wanaishi katika tabia yao potovu, iwapo watu wangekuwa na aina hii ya upendo ama iwapo mtu angeweza kumiliki aina hii ya upendo, bila kuwa na maombi na madai, kuwa radhi kujitoa wenyewe na kuwa radhi kustahimili mateso na kuacha vyote vilivyo vyao, mtu anayemiliki aina hii ya upendo angewezaje kuonekana katika macho ya watu wengine? Si angekuwa mtu kamili? (Ndiyo.) Mtu kamili kama huyo yupo katika dunia hii? Hayupo, yupo? Mtu wa aina hii hayupo kabisa katika dunia hii, ila angeweza kuishi katika utupu, siyo? Hivyo, watu wengine—kupitia uzoefu wao—wanatumia juhudi nyingi kuwa kama kile ambacho maneno haya yalielezea. Wanajishughulikia, wanajizuia, na hata daima wanajitupa: Wanastahimili mateso na wanaacha dhana ambazo si sahihi walizokuwa nazo. Wanaacha njia walivyokuwa wakiasi Mungu, wanaacha tamaa zao na matakwa. Lakini mwishowe bado hawawezi kufikia mahitaji hayo. Kwa nini hayo yanafanyika? Mungu anasema mambo haya ili kupeana kiwango cha watu kufuata, ili watu wajue kiwango wanachodaiwa na Mungu. Lakini Mungu huwahi kusema kwamba watu lazima wafikie hiki mara moja? Je, Mungu huwahi kusema ni katika wakati upi watu wanapaswa kufikia hiki? (La.) Je, Mungu huwahi kusema kwamba watu lazima wampende namna hii? Kifungu hiki kinasema hivi? La, hakisemi hivi. Mungu anawaambia watu tu kuhusu “upendo” Aliokuwa akirejelea. Kuhusiana na watu kuweza kumpenda Mungu namna hii na kumtendea Mungu namna hii, mahitaji ya Mungu ni yapi? Si muhimu kuyafikia mara moja, ama papo hapo kwa sababu watu hawawezi kufanya hivyo. Mmewahi kufikiria kuhusu masharti ambayo watu wanapaswa kutimiza ili kupenda namna hii? Iwapo watu wangeyasoma maneno haya mara nyingi watakuwa na upendo huu polepole? (La.) Masharti ni yapi basi? Kwanza, watu wanawezaje kuwa huru kutokana na tuhuma kumhusu Mungu? (Ni watu waaminifu tu wanaoweza kufikia jambo hilo.) Je, kuwa huru kutokana na udanganyifu? (Pia wanapaswa kuwa watu waaminifu.) Kuwa mmoja asiyetaka kufanya mipango na Mungu? Huyo pia lazima awe mtu mwaminifu, Je, kutokuwa na ujanja? Kunarejelea nini kusema hakuna chaguo katika upendo? Yote yanarejelea kuwa mtu mwaminifu? Kuna maelezo mengi hapo; uwezo wa Mungu kutaja upendo wa aina hii ama uwezo wa Mungu kufafanua aina hii ya upendo, kuisema namna hii, hii inathibitisha nini? Tunaweza kusema kwamba Mungu anamiliki upendo wa aina hii? (Ndiyo.) Mnaona hii wapi? (Kwa upendo Mungu alio nao kwa mwanadamu.) Upendo wa Mungu kwa mwanadamu una sharti? (La.) Kuna vizuizi ama umbali kati ya Mungu na mwanadamu? (La.) Mungu ana tuhuma kumhusu mwanadamu? (La.) Mungu humwangalia mwanadamu, humwelewa mwanadamu, siyo? (Ndiyo.) Mm, kwa kweli anamwelewa mwanadamu. Je, Mungu ni mdanganyifu kwa mwanadamu? (La.) Kwa sababu Mungu anaongea kikamilifu kuhusu upendo huu, moyo Wake ama kiini Chake kinaweza kuwa kamili sana? Watu wamewahi kufafanua upendo kwa njia hii? (La.) Mwanadamu amefafanua upendo katika hali gani? Mwanadamu anazungumza vipi kuhusu upendo? Si ni kupeana ama kutoa? (Ndiyo.) Ufafanuzi wa mwanadamu wa upendo ni rahisi, na hauna kiini.
Ufafanuzi wa Mungu wa upendo na namna Mungu anazungumza kuhusu upendo inahusiana na kipengele cha kiini Chake, lakini kipengele kipi cha kiini Chake? Wakati uliopita Tulishiriki kuhusu mada muhimu sana, ni mada ambayo watu wamezungumzia mara nyingi na kutaja awali, na ni neno ambalo linatajwa mara nyingi katika kipindi cha kumwamini Mungu, lakini ni neno linalojulikana na pia ni geni kwa watu, lakini mbona hivyo? Ni neno linalotoka kwa lugha za mwanadamu, miongoni mwa mwanadamu ufafanuzi wake ni dhahiri na pia ni usio dhahiri, lakini neno hili ni nini? (Utakatifu.) Naam, utakatifu: hiyo ilikuwa mada ya wakati uliopita tuliposhiriki. Tulishiriki kiasi kuhusu mada hii, lakini kushiriki kwetu hakukuwa kamili. Kulingana na sehemu tuliyoshiriki wakati uliopita, kila mtu alipata uelewa mpya kuhusu kiini cha utakatifu wa Mungu? (Ndiyo.) Mnafikiri uelewa mpya ulikuwa nini? Yaani, nini katika uelewa huo ama maneno hayo yaliwafanya kuhisi kwamba uelewa wenu wa utakatifu wa Mungu ulikuwa tofauti ama uliobadilishwa na kile Nilichoshiriki kuhusu utakatifu wa Mungu? Je, mnakumbuka? Je, uliacha maono? (Mungu anasema Anachohisi katika moyo Wake; ni safi. Hiki ni kipengele kimoja cha utakatifu.) Hii ni sehemu moja yake, kuna chochote kingine cha kuongezea? (Kuna utakatifu wakati Mungu ana ghadhabu kwa mwanadamu, hakuna dosari.) (Naona katika mamlaka ya Mungu ukamilifu Wake, uaminifu Wake, hekima Yake na utawala Wake juu ya vitu vyote. Naelewa mambohaya.) “Utawala juu ya vitu vyote,” ambao ni kuhusu mamlaka ya Mungu, sasa tunazungumza kuhusu utakatifu wa Mungu. (Kuhusu utakatifu wa Mungu, naelewa kwamba kuna ghadhabu ya Mungu na huruma ya Mungu katika tabia Yake ya haki, hili liliacha maono yenye nguvu kwangu. Pia lilileta fikira kwamba tabia ya Mungu ya haki ni ya kipekee, ambayo zamani sikuwa na uelewa kama huo wa ama ufafanuzi kama huo wake. Lakini katika ushirika Wako Ulijadili kwamba ghadhabu ya Mungu ni tofauti na hasira ya mwanadamu. Ni kitu ambacho hakuna kiumbe anamiliki. Ghadhabu ya Mungu ni kitu chema na kina kanuni; inatolewa kwa sababu ya kiini kiasilia cha Mungu. Ni kwa sababu Anaona kitu hasi na hivyo Mungu anaachilia ghadhabu Yake. Katika huruma ya Mungu, pia naona kwamba ni kitu ambacho hakuna kiumbe anamiliki. Ingawa mwanadamu ana matendo mazuri ama vitendo vya haki ambavyo vinachukuliwa kuwa sawa na huruma, ni vichafu na kuna nia nyuma yavyo. Aina zingine zinazoitwa huruma hata ni bandia na tupu. Lakini nimeuona wokovu wa Mungu wakati anaonyesha huruma kwa watu, na huruma hii inamweka mwanadamu moja kwa moja kwa njia ya kuokolewa. Inawaweka watu kwa njia sahihi ya kumwamini Mungu ili wapokee hatima na matumaini yao mazuri. Kwa hivyo huruma ya Mungu inamilikiwa na kiini Chake. Kwa hivyo, hata ingawa Mungu angeharibu mji kwa sababu ya ghadhabu Yake, kwa sababu ana kiini cha huruma, Angeweza kwa wakati wowote ama pahali popote kuonyesha huruma kuwaokoa na kuwalinda watu wa mji huo. Huu ni uelewa wangu.) Una baadhi ya uelewa kuhusu tabia ya haki ya Mungu.
Wakati Niliwauliza baadhi ya maswali sasa hivi, wengi wenu walitambua kwamba upendo wa Mungu ni mkubwa sana na halisi sana, lakini hamna maarifa ya kiini takatifu cha Mungu. Kuhusu mada yetu ya sasa, Nitazungumzia eneo hili, ambalo ni maarifa ya utakatifu wa Mungu. Mara nyingi watu huhusisha tabia ya haki ya Mungu na utakatifu Wake na wote wanajua na wamesikia maelezo fulani kuhusu tabia Yake ya haki. Zaidi, watu wengi mara nyingi wanachanganya utakatifu wa Mungu na tabia ya haki katika ushirika wao, wakisema kwamba tabia ya Mungu ya haki ni takatifu. Kila mtu anajua neno “takatifu” na ni neno linalotumika sana, lakini kuhusiana na kidokezo cha neno hilo, maonyesho gani ya utakatifu wa Mungu ambayo watu wanaweza kuona? Ni nini Mungu amefichua ambacho watu wanaweza kutambua? Ninahofia kwamba hiki ni kitu ambacho hakuna anayejua. Tunasema kwamba tabia ya Mungu ni ya haki, lakini basi ukichukua tabia ya haki ya Mungu na kuisema kuwa takatifu, hiyo inaonekana isiyo dhahiri kiasi, ya kuchanganya kiasi; mbona hivi? Unasema tabia ya Mungu ni ya haki, ama unasema tabia Yake ya haki ni takatifu, hivyo katika mioyo yenu mnauainisha utakatifu wa Mungu vipi? Mnauelewa vipi? Hivyo ni kusema, ni nini Mungu amefichua ama ni nini kuhusu kile Mungu anacho na maana Yake ambacho watu wanaweza kutambua kama takatifu? Umefikiria hili hapo awali? Kile Nilichoona ni kwamba watu mara nyingi husema maneno yanayotumika sana ama wana virai ambavyo vimesemwa mara kwa mara, lakini hawajui wanachosema. Hivi tu ni vile kila mtu anavyosema, na wanasema hivi mara nyingi, hivyo inakuwa kirai kilichowekwa. Hata hivyo, iwapo wangechunguza na kutafiti kwa kina maelezo, wangepata kwamba hawajui maana halisi ni nini ama inachorejelea. Kama tu neno “takatifu,” hakuna anayejua kabisa ni kipengele kipi cha kiini cha Mungu kinarejelewa kuhusiana na utakatifu Wake. Kuhusu kupatanisha neno “takatifu” na Mungu, hakuna anayejua na mioyo ya watu imechanganyikiwa, na ni pana jinsi wanavyotambua Mungu ni mtakatifu. Lakini unapoichunguza, Mungu ni mtakatifu vipi? Kuna anayejua? Nahofia hakuna aliye wazi kabisa kuhusu suala hili. Leo tutashiriki kuhusu mada kupatanisha neno “takatifu” na Mungu ili watu waweze kuona maudhui ya kweli ya kiini cha utakatifu wa Mungu, na hili litazuia watu wengine kulitumia neno hilo kimazoea ovyo ovyo na kusema vitu kwa nasibu wakati hawajui maana yake, ama hata kama wako sawa na sahihi ama la. Watu daima wameisema hivi: umeisema, nimeisema, na imekuwa jinsi ya kuongea na watu hivyo wameliharibu neno “takatifu” bila kusudi.
Kuhusu neno “takatifu,” juujuu linaonekana rahisi sana kuelewa, siyo? Kwa kiwango cha chini kabisa watu wanaamini neno “takatifu” linamaanisha nadhifu, isiyo na doa, tukufu, na safi, kama tu katika wimbo tulioimba karibuni “Upendo Safi Bila dosari,” ambapo “takatifu” na “upendo” yamewekwa pamoja, ambayo ni sahihi; hii ni sehemu yake, upendo wa Mungu ni sehemu ya kiini Chake, lakini si kiini chote. Hata hivyo, katika mitazamo ya watu, wanaona neno na kulishirikisha na vitu ambavyo wao wenyewe wanaviona kuwa nadhifu na safi, ama na vitu ambavyo wao binafsi wanafikiri havina doa wala havina dosari. Kwa mfano, watu wengine husema kwamba ua la yungiyungi ni safi, ni vipi watu walikuja kufafanua ua la yungiyungi kwa njia hii? (“Ua la yungiyungi linamea kwa matope lakini linatoa maua bila dosari.”) Linatoa maua bila dosari kutoka kwa maji machafu, hivyo watu wakaanza kutumia neno “takatifu” kwa ua la yungiyungi. Watu wengine pia walichukulia hadithi za mapenzi zilizobuniwa na wengine na yaliyomo ndani kuwa takatifu, ama wangemchukulia mhusika mkuu anayestahili upaa kuwa mtakatifu. Zaidi, wengine walifikiria watu kutoka kwa Biblia, ama wengine walioandikwa katika vitabu vya kiroho—kama watakatifu, mitume, au wengine ambao walimfuata Mungu awali Alipokuwa akifanya kazi Yake—kama waliokuwa na uzoefu wa kiroho ambao ulikuwa takatifu. Haya yote ni mambo yaliyofikiriwa na watu na hizi ni dhana zinazoshikiliwa na watu. Mbona watu wanashikilia dhana kama hizi? Kuna sababu moja na ni rahisi sana: Ni kwa sababu watu wanaishi miongoni mwa tabia potovu na wanaishi katika dunia ya uovu na uchafu. Kila kitu wanachoona, kila kitu wanachogusa, kila kitu wanachopitia ni uovu wa Shetani na upotovu wa Shetani na pia kufanya mipango, kupigana wenyewe kwa wenyewe, na vita vinavyotokea miongoni mwa watu walio chini ya ushawishi wa Shetani. Kwa hivyo, hata wakati Mungu anafanya kazi Yake kwa watu, ama hata wakati Anazungumza na watu na tabia na kiini Chake vyote vinaonyeshwa kwa watu, hawawezi kuona ama kukubali kile ambacho ni utakatifu. Hata zaidi, hii ndiyo sababu watu mara nyingi husema Mungu ni mtakatifu. Kwa sababu watu wanaishi miongoni mwa uchafu na upotovu na wanamilikiwa na Shetani, hawaoni mwangaza na hawajui masuala ama vitu vyema na zaidi, hawajui ukweli. Kwa hivyo, hakuna anayejua maana ya takatifu. Baada ya kusema hayo, kuna vitu vitakatifu ama watu watakatifu miongoni mwa ubinadamu huu potovu? (La.) Tunaweza kusema kwa uhakika kwamba la, hakuna, kwa sababu kiini cha Mungu tu ndicho kitakatifu. Kuhusu utakatifu wa kiini cha Mungu, wakati uliopita tulishiriki kidogo kuuhusu na huo ulikuwa msukumo wa maarifa ya watu ya utakatifu wa Mungu, lakini hautoshi. Hauwezi kutosha kusaidia watu kujua kikamilifu utakatifu wa Mungu, wala hautoshi kuwasaidia kuelewa kwamba utakatifu wa Mungu ni wa kipekee. Zaidi, hautoshi kuruhusu watu kuelewa kipengele cha maana ya ukweli ya utakatifu kwani imejumuishwa kabisa kwa Mungu. Kwa hivyo, ni muhimu kwamba tuendelee ushirika wetu katika mada hii. Katika kifungu cha tatu ushirika wetu ulijadili mada tatu, kwa hivyo sasa tunapaswa kujadili mada ya nne, na tutaanza kusoma maandiko.
4. Majaribu ya Shetani
(Mat 4:1-4) Kisha Yesu akaongozwa na Roho kwenda nyikani ili ajaribiwe na Ibilisi. Na baada ya kufunga siku arobaini mchana na usiku, mwishowe alihisi njaa. Na mjaribu alipomjia, alimwambia, Ukiwa wewe ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. Lakini Yesu akamjibu akasema, Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate peke yake, ila kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Mungu. Haya ndiyo maneno ambayo ibilisi kwanza alijaribu kumjaribu Bwana Yesu. Ni nini maudhui ya aliyoyasema ibilisi? Endelea na uyasome. Ukiwa wewe ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate Ibilisi alisema maneno haya, ambayo yalikuwa rahisi kiasi, lakini kuna shida na maudhui muhimu ya maneno haya? (Ndiyo.) Shida ni nini? Alisema, “Ukiwa wewe ndiwe Mwana wa Mungu” kwa hivyo katika moyo wake, alijua kwamba Bwana Yesu alikuwa Mwana wa Mungu? Alijua kwamba Alikuwa Kristo? (Ndiyo.) Basi kwa nini alisema “ukiwa ndiwe”? (Alikuwa akijaribu kumjaribu Mungu.) Hakika, alikuwa akijaribu kumjaribu Mungu, lakini ni nini madhumuni ya kufanya hivyo? Alisema, “Ukiwa wewe ndiwe Mwana wa Mungu ” Katika moyo wake alijua kwamba Yesu Kristo alikuwa Mwana wa Mungu, haya yalikuwa wazi katika moyo wake, lakini licha ya haya, alinyenyekea Kwake au kumwabudu Yeye? (La.) Alitaka kufanya nini? Alitaka kufanya hivi na kusema maneno haya kumfanya Bwana Yesu kukasirika na kisha kumshawishi kuchukua chambo, na kumdanganya Bwana Yesu kufanya mambo kulingana na njia yake ya kufikiri na kuinuka kwa chango chake. Si alimaanisha hivi? Katika moyo wake alijua wazi kwamba huyu alikuwa Bwana Yesu Kristo, lakini alisema hivi hata hivyo. Hii si asili ya Shetani? Asili ya Shetani ni nini? (Kuwa mjanja, mwovu na kutokuwa na Heshima kwa Mungu.) Hamheshimu Mungu. Ni kitu kipi hasi alichokuwa akifanya hapa? Hakutaka kumshambulia Mungu? Alitaka kutumia mbinu hii kumshambulia Mungu, alisema: “Ukiwa wewe ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate .”); si hii ni nia ovu ya Shetani? (Ndiyo.) Alikuwa anajaribu kufanya nini kweli? Lengo lake ni wazi sana: Alikuwa anajaribu kutumia mbinu hii kukanusha nafasi na utambulisho wa Bwana Yesu Kristo. Alisema, “Ukiwa ndiwe Mwana wa Mungu, amuru kwamba mawe haya yawe mikate. Usipo, basi wewe siwe Mwana wa Mungu na Hufanyi kazi hii.” Ni haya yaliyomaanishwa hapa? Alitaka kutumia mbinu hii kumshambulia Mungu, alitaka kuvunja na kuharibu kazi ya Mungu; huu ndio uovu na ujanja wa Shetani. Uovu wake ni maonyesho ya kiasili ya asili yake. Ingawaje alijua Bwana Yesu Kristo alikuwa Mwana wa Mungu, kupata mwili kwenyewe kwa Mungu Mwenyewe, hangeweza kuwacha kufanya kitu kama hiki, kumfuata Mungu nyuma na kuendelea kumshambulia na kujaribu sana kuvuruga na kuharibu kazi ya Mungu na kumfanya Mungu kuwa adui.
Sasa, hebu tuchambue kirai hiki alichotumia Shetani: “amuru kwamba mawe haya yawe mikate” Kubadili mawe yawe mikate—hili linamaanisha chochote? Halina maana. Iwapo kuna chakula, mbona usile? Mbona ni muhimu kubadili mawe yawe mikate? Kuna maana hapa? (La.) Ingawa alikuwa amefunga wakati huo, kwa hakika Bwana Yesu alikuwa na chakula cha kula? Je, Alikuwa na chakula? (Alikuwa nacho.) Kwa hivyo, hapa, tunaona upuuzi wa matumizi ya Shetani ya kirai hiki. Kwa usaliti na uovu wake wote, tunaona upuuzi na ujinga wake, siyo? Shetani anafanya idadi fulani ya mambo. Unaona asili yake ovu na unaona akiharibu kazi ya Mungu. Ni wa kuchukiza na kuudhi. Lakini kwa upande mwingine, unapata asili ya kitoto na ujinga nyuma ya maneno na vitendo vyake? (Ndiyo.) Huu ni ufunuo kuhusu asili ya Shetani; ana asili ya aina hii na atafanya kitu kama hiki. Kwa wanadamu, kirai hiki ni cha upuuzi na cha kuchekesha. Lakini maneno kama hayo kwa hakika yanaweza kutamkwa na Shetani. Tunaweza kusema kwamba ni asiyejua? Mjinga? Uovu wa Shetani uko kila mahali na daima unafichuliwa. Na Bwana Yesu anamjibu aje? (“Mtu hataishi kwa mkate peke yake, ila kwa kila neno linalotoka katika kinywa cha Mungu ”) Maneno haya yana nguvu yoyote? (Yanayo.) Mbona tunasema kwamba yana nguvu? (Ni ya ukweli.) Sahihi. Maneno haya ni ukweli. Sasa, mtu anaishi kwa mkate tu? Bwana Yesu alifunga kwa siku na usiku 40. Alikufa kwa njaa? (La.) Hakufa kwa njaa, kwa hivyo Shetani alimkaribia, akimwambia abadili mawe yawe chakula kwa kusema kitu kama hiki: Ukiyabadili mawe yawe chakula, Hutakuwa basi na vitu vya kula? Si basi Hutalazimika kufunga, Hutalazimika kuwa na njaa? Lakini Bwana Yesu alisema, Mtu hataishi kwa mkate peke yake inayomaanisha kwamba, ingawa mwanadamu anaishi katika mwili, kile kinachompa uhai, kile kinachouruhusu mwili wake kuishi na kupumua, si chakula, ila maneno yote yaliyotamkwa na kinywa cha Mungu. Katika upande mmoja, mwanadamu anachukulia maneno haya kuwa ukweli. Maneno haya yanampa imani, yanamfanya ahisi kwamba anaweza kumtegemea Mungu, kwamba Mungu ni ukweli. Kwa upande mwingine, kuna kipengele cha vitendo katika maneno haya? (Kunacho.) Mbona? Kwa sababu Bwana Yesu amefunga kwa siku na usiku 40 na bado Anasimama hapo, bado ako hai. Huu ni mfano? Cha maana hapa ni kwamba Hajakula chochote, chakula chochote kwa siku na usiku 40. Bado ako hai. Huu ni ushahidi wa nguvu nyuma ya kirai Chake. Kirai hiki ni rahisi, lakini, kuhusiana na Bwana Yesu, Alifunzwa kirai hiki na mtu mwengine, ama Alikifikiria tu kwa sababu ya kile Shetani alimwambia? Fikiria jambo hili. Mungu ni ukweli. Mungu ni uhai. Je, ukweli na uhai wa Mungu uliongezwa kwa kuchelewa? Ulitokana na uzoefu? (La.) Ni ya asili ndani ya Mungu, kumaanisha kwamba ukweli na uhai vipo ndani ya kiini cha Mungu. Licha ya kile kinachomfanyikia, Anachofichua ni ukweli. Ukweli huu, kirai hiki—iwapo maudhui yake ni ndefu ama fupi—kinaweza kumwacha mwanadamu aishi, kimpe uhai; kinaweza kumwezesha mwanadamu kupata, ndani yake, ukweli, uwazi kuhusu safari ya maisha, na kumwezesha kuwa na imani kwa Mungu. Hiki ndicho chanzo cha matumizi ya Mungu ya kirai hiki. Chanzo ni chema, kwa hivyo kitu hiki chema ni takatifu? (Ndiyo.) Kirai cha Shetani kinatoka kwa asili ya Shetani. Shetani anafichua asili yake ovu, asili yake yenye kijicho, kila mahali, daima. Sasa, ufunuo huu, anaufanya kiasili? (Ndiyo.) Kuna yeyote anayemchochea? Kuna yeyote anayemsaidia? Kuna yeyote anayemshurutisha? (La.) Anautoa kwa hiari yake mwenyewe. Hii ni asili ovu ya Shetani. Licha ya kile Mungu anafanya na jinsi Anavyokifanya, Shetani ako nyuma Yake. Kiini na sura ya ukweli ya vitu hivi ambavyo Shetani anasema na kufanya ni kiini cha Shetani—kiini ovu, kiini cha kuonea kijicho. Sasa, kuendelea kusoma, ni nini tena Shetani anasema? Tuendelee kusoma hapa chini.
(Mat 4:5-6) Kisha Ibilisi akamchukua hadi mji mtakatifu, na kumweka juu ya kinara cha hekalu, Na akamwambia, Ukiwa wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini: kwa maana imeandikwa,
Atawaagiza malaika wake wakuchunge: Na mikononi mwao watakubeba, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe wakati wowote.
Hebu kwanza tuzungumze kuhusu kirai hiki cha Shetani. Alisema “Ukiwa wewe ndiwe Mwana wa Mungu, jitupe chini ,” na kisha akadondoa kutoka kwa maandiko, “Atawaagiza malaika wake wakuchunge: Na mikononi mwao watakubeba, usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe wakati wowote .” Unahisi vipi unaposikia maneno ya Shetani? Si ni ya kitoto sana? Ni ya kitoto, upuuzi na kuchukiza. Mbona Nasema hivi? Daima Shetani hufanya kitu kijinga, anaamini kwamba ni mwerevu sana; na mara nyingi hutaja maandiko—hata neno la Mungu—anajaribu kuyabadili maneno haya dhidi ya Mungu kumshambulia na kumjaribu. Lengo lake la kufanya hivi ni kuharibu mpango wa kazi ya Mungu. Hata hivyo, unaona chochote kwa kile Shetani amesema? (Kuna nia mbaya hapo.) Shetani daima amekuwa mjaribu; haongei kwa njia inayoeleweka rahisi, huongea kwa njia isiyo wazi akitumia majaribu, ulaghai na ushawishi. Shetani anamjaribu Mungu na pia mwanadamu: Anafikiri kwamba Mungu na mwanadamu wote hawajui, ni wajinga, na hawawezi kutofautisha kwa wazi vitu vilivyo. Shetani anafikiri kwamba Mungu na pia mwanadamu hawataona hadi kwa kiini chake na kwamba Mungu na mwanadamu wote hawataona ujanja wake na nia zake mbaya. Si hapa ndipo Shetani anapata ujinga wake? (Ndiyo.) Zaidi, Shetani anataja maandiko wazi; anafikiria kwamba kufanya hivyo kunamfanya kuaminika, na kwamba hutaweza kuona dosari zozote kwa haya ama kuepuka kudanganywa na haya. Si hapa ndipo Shetani anakuwa mjinga na kama mtoto? (Ndiyo.) Hii ni kama wakati watu wengine wanaeneza injili na kuwa na ushuhuda kwa Mungu, si wasioamini watasema kitu kama alichosema Shetani? Umesikia watu wakisema kitu kama hiki? (Ndiyo.) Unahisi kuchukizwa unaposikia vitu kama hivyo? (Ndiyo,) Unapohisi kuchukizwa, pia unahisi kutiwa kinyaa na kukirihishwa? (Ndiyo.) Unapokuwa na hisia hizi unaweza kutambua kwamba Shetani na tabia potovu ambayo Shetani anamfanyia mwanadamu ni ovu? Katika mioyo yenu mmewahi kuwa na utambuzi kama, “Mungu kamwe haongei namna hiyo. Maneno ya Shetani yanaleta mashambulizi na majaribu, maneno yake ni ya ujinga, ya kuchekesha, ya kitoto, na ya kuchukiza. Hata hivyo, katika matamshi ya Mungu na vitendo vya Mungu, Hangetumia mbinu kama hizi kuzungumza ama kufanya kazi Yake, na Hajawahi kufanya hivyo”? Bila shaka, katika hali hii watu wana tu kiasi kidogo cha kuhisi kuendelea na hawana utambuzi wa utakatifu wa Mungu; wanaweza tu kukubali kwamba neno la Mungu ni ukweli, lakini hawajui kwamba ukweli ni utakatifu wenyewe. Na kimo chenu cha sasa, mnahisi tu hivi: “Kila kitu Mungu anasema ni ukweli, ni cha manufaa kwetu, na lazima tukikubali”; bila kujali iwapo unaweza kukubali hili au la, bila ubaguzi unasema kwamba maneno ya Mungu ni ukweli na kwamba Mungu ni ukweli, lakini hujui kwamba ukweli ni utakatifu wenyewe na kwamba Mungu ni mtakatifu. Hivyo, jibu la Yesu kwa maneno ya Shetani lilikuwa lipi?
(Mat 4:7) Yesu akamwambia, Imeandikwa tena, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
Kuna ukweli katika kirai hiki ambacho Yesu alisema? (Ndiyo.) Kuna ukweli kwa kirai hicho. Juujuu inaonekana kama amri ya watu kufuata, ni kirai rahisi sana, lakini ni kimoja ambacho mwanadamu na Shetani wamekiuka mara nyingi. Hivyo, Bwana alimwambia, “Usimjaribu Bwana Mungu wako.” kwa sababu hiki ndicho kile Shetani alifanya mara nyingi na alifanya kila juhudi kufanya hivyo, unaweza hata kusema kwamba Shetani alifanya hivyo bila haya. Ni asili ya msingi ya Shetani kutomcha Mungu na kutomheshimu Mungu kwa moyo wake. Hivyo, hata wakati Shetani alikuwa kando ya Mungu na angeweza kumwona, Shetani hakuweza kuacha kumjaribu Mungu. Kwa hivyo, Bwana Yesu alimwambia Shetani, “Usimjaribu Bwana Mungu wako.” Hiki ni kirai ambacho Mungu amemwambia Shetani mara nyingi. Si kutumia kirai hiki kunafaa hata leo? (Ndiyo.) Mbona? (Kwa sababu pia sisi humjaribu Mungu mara nyingi.) Watu mara nyingi humjaribu Mungu, lakini mbona watu hufanya hivyo mara nyingi? Je, ni kwa sababu watu wamejawa na tabia potovu ya kishetani? (Ndiyo.) Kwa hivyo kile Shetani alisema hapa juu ni kitu ambacho watu husema mara nyingi? (Ndiyo.) Katika hali gani? Mtu anaweza kusema kwamba watu wamekuwa wakisema mambo kama haya na kuyafichua kiasili licha ya wakati na mahali. Hii inadhihirisha kwamba tabia ya watu ni sawa kabisa na tabia potovu ya Shetani. Bwana Yesu alisema kirai rahisi, ambacho kinawakilisha ukweli na ambacho watu wanahitaji. Hata hivyo, katika hali hii Bwana Yesu alikuwa akigombana na Shetani? Kulikuwa na chochote cha kukabiliana kwa kile Alisema kwa Shetani? (La.) Bwana Yesu aliyachukulia vipi majaribu ya Shetani kwa moyo Wake? Je, Alihisi kuchukizwa na kutiwa kinyaa? (Ndiyo.) Bwana Yesu alihisi kutiwa kinyaa na kuchukizwa lakini Hakugombana na Shetani, wala hata chini zaidi Hakuzungumza kuhusu kanuni zozote kubwa, sivyo? (Ndiyo.) Mbona hivyo? (Bwana Yesu hakutaka kumkiri Shetani.) Kwa nini Hakutaka kumkiri Shetani? (Kwa sababu Shetani daima ako hivyo, hawezi kubadilika.) Tunaweza kusema kwamba Shetani hana akili? (Ndiyo, tunaweza.) Je, Shetani anaweza kutambua kwamba Mungu ni ukweli? Shetani hatawahi kutambua kwamba Mungu ni ukweli na hatawahi kukubali kwamba Mungu ni ukweli; hii ni asili yake. Zaidi, kuna kitu kingine kuhusu asili ya Shetani kinachotia watu kinyaa, ni nini? Katika majaribio yake ya kumjaribu Bwana Yesu, aliamini nini katika moyo wake? Hata kama alimjaribu Mungu na hangefaulu, ila Shetani alijaribu tu. Hata kama angeadhibiwa, aliifanya tu. Hata kama hangepata chochote chema kutoka kwa kufanya hivyo, aliifanya tu, na kuendelea na kusimama dhidi ya Mungu hadi mwisho kabisa. Hii ni asili ya aina gani? Si huo ni uovu? (Ndiyo.) Yule anayekasirika sana wakati Mungu anatajwa, amemwona Mungu? Yule anayekuwa na hasira wakati Mungu anatajwa, anamjua Mungu? Hajui Mungu ni nani, hamwamini, na Mungu hajamwongelesha. Mungu hajawahi kumsumbua, kwa hivyo mbona akuwe na hasira? Tunaweza kusema kwamba mtu huyu ni mwovu? (Ndiyo.) Huyu anaweza kuwa mtu mwenye asili ovu? Haijalishi ni mienendo gani inafanyika duniani, iwe ya kufurahisha, chakula, watu maarufu, watu wenye sura nzuri, hakuna yoyote haya yanayomsumbua, lakini kutajwa mara moja kwa neno “Mungu” na anakasirika; huu si mfano wa asili ovu? Huu unatumika kama ushahidi wa kuridhisha wa asili ovu ya mwanadamu. Sasa, mkijizungumzia, kuna wakati ambapo ukweli unatajwa, ama wakati majaribio ya Mungu kwa mwanadamu yanatajwa ama wakati maneno ya Mungu ya hukumu dhidi ya mwanadamu yanatajwa, na mnahisi kusumbuliwa, kutiwa kinyaa, na hamtaki kusikia kuyahusu? Mioyo yenu inaweza kufikiri: Huu ni ukweli vipi? Si watu wote walisema kwamba Mungu ni ukweli? Huu si ukweli, haya bila shaka ni maneno ya Mungu ya maonyo kwa mwanadamu! Watu wengine hata wanaweza kuhisi kuchukizwa kwa mioyo yao: Haya yanatajwa kila siku, majaribio Yake kwetu yanatajwa kila siku kama hukumu Yake; haya yote yataisha lini? Tutapokea lini hatima njema? Haijulikani hasira hii isiyo na busara inatoka wapi. Hii ni asili ya aina gani? (Asili ovu.) Inasababishwa na asili ovu ya Shetani. Na kwa Mungu kuhusu asili ovu ya Shetani na tabia potovu ya mwanadamu, Hagombani kamwe wala kubishana na watu, na kamwe Halalamiki wakati watu wanatenda kutokana na ujinga. Hamtamwona Mungu akiwa na mitazamo sawa kuhusu vitu ambavyo watu wanavyo, na zaidi hamtamwona Akitumia maoni ya wanadamu, maarifa yao, sayansi yao ama filosofia yao ama fikira za mwanadamu kushughulikia vitu, Badala yake, kila kitu anachofanya Mungu na kila kitu Anachofichua kinahusiana na ukweli. Yaani, kila neno ambalo amesema na kila kitendo amefanya kinahusiana na ukweli. Ukweli huu sio tu ndoto isiyo na msingi; ukweli huu na maneno haya yanaelezwa na Mungu kwa sababu ya kiini cha Mungu na uhai Wake. Kwa sababu maneno haya na kiini cha kila kitu Mungu amefanya ni ukweli, hivyo tunaweza kusema kwamba kiini cha Mungu ni kitakatifu. Kwa maneno mengine, kila kitu ambacho Mungu anasema na kufanya kinaleta uzima na mwangaza kwa watu, kinawaruhusu watu kuona vitu vyema na uhalisi wa vitu hivi vyema na kuashiria ubinadamu kwa njia ya mwangaza ili waweza kutembea njia njema. Vitu hivi vinaamuliwa kwa sababu ya kiini cha Mungu na vinaamuliwa kwa sababu ya kiini cha utakatifu Wake. Mmekiona, siyo? Tutaendelea kuyasoma maandiko. .
(Mat 4:8-11) Tena, Ibilisi akamchukua hadi kwenye mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na utukufu wao; Na akamwambia, Hivi vyote nitakupa, ukianguka chini na kuniabudu. Kisha Yesu akamwambia, Ondoka uende zako, Shetani; kwa kuwa imeandikwa, Muabudu Bwana Mungu wako, na ni yeye peke yake utakayemtumikia. Basi Ibilisi akamwacha, na, tazama, malaika wakaja na wakamhudumia. Shetani, ibilisi, baada ya kushindwa katika hila zake mbili za awali, alijaribu nyingine tena: Alionyesha falme zote duniani na utukufu wa falme hizi kwa Bwana Yesu na kumwambia amwabudu ibilisi. Unaona nini kuhusu sura za ukweli za ibilisi kutoka kwa hali hii? Si Shetani ibilisi hana haya kabisa? (Ndiyo.) Anaweza kukosa haya namna gani? Kila kitu kiliumbwa na Mungu, lakini Shetani anakigeuza na kumwonyesha Mungu akisema, “Hivi vyote nitakupa, ukianguka chini na kuniabudu.” Je, si hili ni mabadiliko ya jukumu? Si Shetani hana haya? Mungu aliumba kila kitu, lakini kilikuwa cha raha Zake? Mungu alimpa mwanadamu kila kitu, lakini Shetani alitaka kunyakua vyote na baadaye akasema, “Niabudu! Niabudu na ntakupa Wewe haya yote.” Huu ni uso usiopendeza wa Shetani; hana haya kabisa, siyo? Shetani hata hajui maana ya neno “haya,” na huu ni mfano mwingine tu wa uovu wake. Hata hajui “haya” ni nini. Shetani anajua vyema kwamba Mungu aliumba kila kitu na kwamba Anavisimamia na Anavitawala. Kila kitu ni cha Mungu, si cha mwanadamu, sembuse Shetani, lakini Shetani ibilisi bila haya alisema kwamba angempa Mungu kila kitu. Si tena Shetani anafanya kitu cha ujinga na kisicho na aibu? Mungu anamchukia Shetani hata zaidi sasa, siyo? Lakini licha ya kile Shetani alijaribu kufanya, Bwana Yesu alikiamini? (La.) Bwana Yesu alisema nini? (“Muabudu Bwana Mungu wako,.”) Je, kirai hiki kina maana ya utendaji? (Ndiyo.) Maana gani ya utendaji? Tunaona uovu na kutokuwa na aibu kwa Shetani katika matamshi yake. Kwa hivyo iwapo mwanadamu angemwabudu Shetani, hitimisho lingekuwa nini? Angepokea utajiri na utukufu wa falme zote? (La.) Angepokea nini? Je, wanadamu wangekuwa wasio na haya na wa kuchekwa kama tu Shetani? (Ndiyo.) Hawangekuwa tofauti na Shetani basi. Kwa hivyo, Bwana Yesu alisema kirai hiki ambacho ni muhimu kwa kila mtu: “Muabudu Bwana Mungu wako, na ni yeye peke yake utakayemtumikia,” kinachosema kwamba isipokuwa Bwana, isipokuwa Mungu Mwenyewe, ukimhudumia mwengine, ukimwabudu Shetani ibilisi, basi utagaagaa katika uchafu sawa na Shetani. Kisha utashiriki kutokuwa na haya na uovu wa Shetani, na kama tu Shetani ungemjaribu Mungu na kumshambulia Mungu. Na basi mwisho wako ungekuwa upi? Ungechukiwa na Mungu, kufilishwa na Mungu na kuangamizwa na Mungu, sivyo? Baada ya Shetani kumjaribu Bwana Mungu mara kadhaa bila mafanikio, alijaribu tena? Shetani hakujaribu tena na kisha akaondoka. Hii inathibitisha nini? Inathibitisha kwamba asili ovu ya Shetani, kuonea kijicho kwake, na ujinga na upuuzi wake yote hayastahili kutajwa mbele ya Mungu kwa sababu Bwana Yesu alimshinda Shetani kwa sentensi tatu tu, na baadaye akatoroka na mkia wake katikati ya miguu yake, kuaibika sana asiweze kuonyesha uso wake tena, na hakumjaribu Yeye tena. Kwa sababu Bwana Yesu alikuwa amelishinda jaribio hili la Shetani, Angeweza kuendelea kwa urahisi kazi ambayo Alipaswa kufanya na kuanza kazi zilizokuwa mbele Yake. Je, yote aliyoyasema Bwana Yesu na kufanya katika hali hii yanabeba maana kiasi ya vitendo kwa kila mtu yakitumika sasa? (Ndiyo.) Maana ya utendaji ya aina gani? Je, kumshinda Shetani ni kitu rahisi kufanya? (La.) Ingekuwa nini basi? Ni lazima watu wawe na uelewa wazi wa asili ovu ya Shetani? Ni lazima watu wawe na uelewa sahihi wa majaribu ya Shetani? (Ndiyo.) Ukiwahi kupitia majaribu ya Shetani katika maisha yako, na iwapo unaweza kuona hadi kwa asili ovu ya Shetani, utaweza kumshinda? Iwapo unajua kuhusu ujinga na upuuzi wa Shetani, bado unaweza kusimama kando ya Shetani na kumshambulia Mungu? (La, hatungeweza.) Ikiwa unaelewa jinsi kuwa na kijicho na kutokuwa na aibu kwa Shetani vinafichuliwa kupitia kwako—iwapo unatambua wazi na kujua mambo haya—bado ungemshambulia na kumjaribu Mungu kwa njia hii? (La, hatungeweza.) Utafanya nini? (Tutaasi dhidi ya Shetani na kumwacha.) Hili ni jambo rahisi kufanya? (La.) Hili si rahisi, kufanya hivi, watu wanalazimika kuomba mara nyingi, ni lazima wajiweke mbele ya Mungu, na lazima wajichunguze. Lazima watii nidhamu ya Mungu na hukumu Yake na kuadibu Kwake na kwa njia hii tu ndipo watu wataweza kujitoa polepole kutoka kwa utawala na udhibiti wa Shetani.
Tunaweza kuweka pamoja mambo yanayojumuisha kiini cha Shetani kutoka kwa mambo haya ambayo amesema. Kwanza, kiini cha Shetani kwa jumla kinaweza kusemwa kuwa ovu, ambacho ni kinyume na utakatifu wa Mungu. Kwa nini Nasema kiini cha Shetani ni ovu? Mtu anapaswa kuangalia matokeo ya kile Shetani anafanyia watu ili kuona haya. Shetani anapotosha na kudhibiti mwanadamu, na mwanadamu anatenda chini ya tabia potovu ya Shetani, na anaishi katika dunia iliyopotoshwa na Shetani na kuishi miongoni mwa watu potovu. Wengi wanamilikiwa na kusimilishwa na Shetani bila kusudi na mwanadamu hivyo ana asili ovu ya Shetani. Kutoka kwa yote Shetani amesema na kufanya, tunaweza kuona kiburi chake na kuona ujanja na kijicho chake. Kiburi cha Shetani kimsingi kinaonekana vipi? Je, Shetani daima anataka kuchukua nafasi ya Mungu? Shetani daima anataka kuharibu kazi ya Mungu na nafasi ya Mungu na kuyachukua kuwa yake ili watu waunge mkono na kuabudu Shetani; hii ni asili ya kiburi ya Shetani. Lakini wakati Shetani anapotosha watu, anafanya hivyo kwa njia ya ujanja na ya usaliti: Wakati Shetani anafanya kazi yake kwa watu, hawaambii watu moja kwa moja jinsi ya kumkataa na kumpinga Mungu. Wakati Shetani anamjaribu Mungu, hatoki na kusema, “Nakujaribu, nitakushambulia,” hivyo Shetani anatumia mbinu gani? (Ushawishi.) Anashawishi, anajaribu, anashambulia, na anaweka mitego yake, na hata kwa kutaja maandiko, Shetani anazungumza na kutenda kwa njia mbalimbali ili kutimiza nia zake mbaya. Baada ya Shetani kufanya hivi, ni nini kinachoweza kuonekana kutoka kile kilichojitokeza kwa mwanadamu? Je, si watu wana kiburi? Mwanadamu ameteseka kutoka kwa upotovu wa Shetani kwa maelfu ya miaka na hivyo mwanadamu amekuwa mwenye kiburi na mwenye majivuno mengi sana, na amekuwa mjanja, mwenye kijicho, na asiyefikiri, siyo? Haya mambo yote yametokana kwa sababu ya asili ya Shetani. Kwa sababu asili ya Shetani ni ovu, amempa mwanadamu asili hii ovu na kumletea mwanadamu tabia hii potovu. Kwa hivyo, mwanadamu anaishi chini ya tabia potovu ya kishetani na, kama Shetani, mwanadamu anaenda kinyume na Mungu, anamshambulia Mungu, na kumjaribu Yeye hadi kwa kiwango ambacho mwanadamu hamwabudu Mungu na hamheshimu katika moyo wake, siyo?
Kuhusu utakatifu wa Mungu, hata kama inaweza kuwa mada inayojulikana, katika majadiliano inaweza kuwa dhahania kiasi kwa watu wengine, na maudhui yake yanaweza kuwa ya kina sana. Zamani, watu hawakushughulika sana na mada ya utakatifu wa Mungu, kwa hivyo hawaielewi. Lakini msijali, Nitawasaidia kuelewa maana ya utakatifu wa Mungu. Naona kwamba ni vigumu kidogo kwenu kupokea, wacha tuseme hili kwanza: Iwapo unataka kujua mtu, angalia tu kile anachofanya na matokeo ya vitendo vyake, na utaweza kuona kiini cha mtu huyo. Kwa hivyo hebu tushiriki kuhusu utakatifu wa Mungu kutoka kwa mtazamo huu kwanza. Tulisema kwamba kiini cha Shetani ni ovu na chenye kijicho, na kwa hivyo vitendo vya Shetani kwa mwanadamu vimekuwa kumpotosha bila kikomo. Shetani ni mwovu, kwa hivyo watu ambao amepotosha hakika ni waovu, siyo? Kuna yeyote anayeweza kusema, “Shetani ni mwovu, pengine mtu aliyepotosha ni mtakatifu”? Ni mzaha, siyo? Je, hata inawezekana? (La.) Kwa hivyo usimfikirie hivyo, wacha tumzungumzie kutoka kwa kipengele hiki: Shetani ni mwovu, hiki ni kiini chake na ni halisi, haya si mazungumzo matupu tu. Hatujaribu kusema uwongo juu ya Shetani; tunashiriki tu kuhusu ukweli na uhalisi na pia kuhusu ukweli unaomzunguka. Hii inaweza kuumiza watu wengine ama sehemu fulani ya watu, lakini hakuna nia mbaya hapa; pengine mtasikia haya leo na kuhisi kutostareheka kiasi, lakini siku fulani hivi punde, wakati mnaweza kumtambua, mtajichukia, na mtahisi kwamba kile tulichozungumzia leo ni cha manufaa kwenu na chenye thamani.

Chanzo: Kanisa la Mwenyezi Mungu
Yaliyopendekezwa: Umeme wa Mashariki

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni