Alhamisi, 31 Mei 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Siri ya Utauwa: Mfuatano" (5) | Kufahamu Umuhimu wa Mungu Kupata Mwili Mara Mbili

"Siri ya Utauwa: Mfuatano" (5) | Kufahamu Umuhimu wa Mungu Kupata Mwili Mara Mbili

Kupata mwili wa Mungu wa kwanza Alipigiliwa misumari msalabani, hivyo kuhitimisha kazi ya kuwakomboa wanadamu. Katika siku za mwisho, kupata mwili wa Mungu wa pili anaonyesha ukweli na Anafanya kazi Yake ya hukumu na kuadibu, Akiwaokoa wanadambu kabisa kutoka kwa miliki ya Shetani. Mungu kupata mwili mara mbili kuna umuhimu mkuu, kama tu anavyosema Mwenyezi Mungu, "Yesu alifanya hatua ya kazi ambayo ilitimiza tu kiini cha "Neno alikuwako kwa Mungu": Ukweli wa Mungu ulikuwako kwa Mungu, na Roho wa Mungu alikuwa na mwili na alikuwa asiyetenganishwa kutoka Kwake, yaani, mwili wa Mungu mwenye mwili ulikuwa na Roho wa Mungu, ambalo ni thibitisho kuu zaidi kwamba Yesu mwenye mwili alikuwa aliyepata mwili wa kwanza wa Mungu. Hatua hii ya kazi ilitimiza maana ya ndani ya "Neno lapata mwili," ilichangia kwenye maana ya kina zaidi ya "naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu,’…” (Neno Laonekana Katika Mwili).

70. Kazi ya Mungu ni Ya Hekima Sana!

Shiji    Jiji la Ma’anshan , Mkoa wa Anhui
Wakati wa kufanya kazi kwangu kama kiongozi katika kanisa, kiongozi wangu mara nyingi angeshirikiana mifano ya kushindwa kwa wengine ili kutumikia kama somo kwetu. Kwa mfano: Viongozi wengine walizungumza tu kuhusu elimu na mafundisho lakini walikosa kutaja upotovu wao au kuwasiliana kwa karibu kuhusiana na ufahamu wao wa jinsi ukweli unavyotumika kwa ukweli. Kama matokeo, viongozi kama hao mara nyingi hawakuwa na ufanisi katika miaka yao ya utumishi na hata wakawa wale ambao hufanya uovu na kumpinga Mungu. Viongozi wengine wangejionyesha, kujiinua na kujishuhudia wenyewe ili kulinda hadhi yao. Mwishowe, viongozi hao wangekuwa wapinga Kristo, wakiwaleta wadogo wao mbele yao katika mashindano ya wazi na Mungu. Viongozi wengine, wakati wa kazi yao, wangeonyesha nadhari kubwa mno kwa miili yao wenyewe, wakitamani wasaa wa burudani na bila kufanya kazi yoyote halisi kamwe. Viongozi hao walikuwa kama vimelea wanaotegemea faida za hadhi ya kanisa. Hatimaye, walifichuliwa na kuondoshwa. …

Jumatano, 30 Mei 2018

"Siri ya Utauwa: Mfuatano" (4) - Kwa Nini Mungu Anakuwa Mwili Mara Mbili ili Kuwaokoa Wanadamu

"Siri ya Utauwa: Mfuatano" (4) - Kwa Nini Mungu Anakuwa Mwili Mara Mbili ili Kuwaokoa Wanadamu

Katika Enzi ya Neema, Mungu mwenye mwili alipigiliwa misumari msalabani, Akazichukua dhambi za mwanadamu na kukamilisha kazi ya kuwakomboa wanadamu. Katika siku za mwisho, Mungu kwa mara nyingine Amepata mwili kuonyesha ukweli na kumtakasa na kumwokoa mwanadamu kabisa. Hivyo kwa nini Mungu anahitaji kupata mwili mara mbili ili kufanya kazi ya wokovu wa mwanadamu? Mwenyezi Mungu asema, "Kupata mwili mara ya kwanza kulikuwa kumkomboa mwanadamu kutoka katika dhambi kupitia mwili wa Yesu, hivyo, Aliokoa mwanadamu kutoka kwa msalaba, lakini tabia potovu ya kishetani ilibaki ndani ya mwanadamu. Kupata mwili mara ya pili si kwa ajili ya kuhudumu tena kama sadaka ya dhambi ila ni kuwaokoa kamilifu wale waliokombolewa kutoka kwa dhambi. Hii inafanyika ili wale waliosamehewa wakombolewe kutoka kwa dhambi zao, na kufanywa safi kabisa, na kupata mabadiliko ya tabia, hivyo kujikwamua kutoka kwa ushawishi wa Shetani wa giza na kurudi mbele za kiti cha enzi cha Mungu. Hivyo tu ndivyo mwanadamu ataweza kutakaswa kikamilifu. ... Kupatikana kwa mwili mara ya pili kunatosha kumaliza dhambi za mwanadamu na kumtakasa mwanadamu. Hivyo, kupatikana kwa mwili mara ya pili kutafikisha tamati kazi yote ya Mungu mwenye mwili na kukamilisha umuhimu wa Mungu kupata mwili" (Neno Laonekana Katika Mwili).

67. Zawadi ya Kupendeza Zaidi Ambayo Mungu Amenipa

Yixin    Jiji la Shijiazhuang, Mkoa wa Hebei
Kabla, ningewasikia mara kwa mara ndugu zangu wa kiume na wa kike wakisema, "Kila kitu ambacho Mungu hufanya ni kwa ajili ya matokeo mazuri; ndiyo yote wanayohitaji watu." Nilikubali hili na kukubaliana nalo, lakini sikuwa na ufahamu wowote kupitia uzoefu wangu mwenyewe. Baadaye nilipata ufahamu kiasi kwa njia ya mazingira ambayo Mungu aliniumbia.
Nilikuwa na hamu kubwa hasa ya hadhi katika moyo wangu. Daima nilikuwa na matumaini kwamba kiongozi angenisikiliza na kwamba ndugu zangu wa kiume na wa kike wangeniheshimu, lakini uhalisi haukuwa kamwe kama nilivyotarajia ungekuwa. Kwa kipindi cha miaka kadhaa, bila kujali ni nani niliyeshirikiana naye wakati wa kutimiza wajibu wangu, nilikuwa "msaidizi" daima. Bila kujali ni nini kilichokuwa kikiendelea, kiongozi angekijadili na mshirika wangu daima na kumpangia kushughulikia mambo.

Jumanne, 29 Mei 2018

"Siri ya Utauwa: Mfuatano" (3) - Tofauti Kati ya Ubinadamu wa Kawaida wa Kristo na Ubinadamu wa Wanadamu wapotovu

"Siri ya Utauwa: Mfuatano" (3) - Tofauti Kati ya Ubinadamu wa Kawaida wa Kristo na Ubinadamu wa Wanadamu wapotovu

Mungu anapata mwili kumwokoa mwanadamu na, kutoka nje, Mungu mwenye mwili Anaonekana kuwa mtu wa kawaida. Lakini je, wajua tofauti muhimu kati ya ubinadamu wa kawaida wa Mungu mwenye mwili na ubinadamu wa wanadamu wapotovu? Mwenyezi Mungu asema, "Mwili uliovaliwa na Roho wa Mungu ni mwili wa Mungu mwenyewe. Roho wa Mungu ni mkubwa, Yeye ni mwenyezi, mtakatifu, na mwenye haki—na vilevile ndivyo ambavyo mwili Wake ulivyo pia mkubwa, wenye uwezo, mtakatifu, na wenye haki. ... licha ya ukweli kwamba mwanadamu na Kristo wanakaa mahala pamoja, ni mwanadamu tu ndiye ambaye anatawaliwa, anatumiwa, na kutegwa na Shetani. Kinyume cha hayo, Kristo daima hapenyezwi na uovu wa Shetani, kwa kuwa Shetani hataweza kamwe kupaa hadi mahala pa aliye juu zaidi, na hataweza kumkaribia Mungu" (Neno Laonekana Katika Mwili).

Jumatatu, 28 Mei 2018

"Siri ya Utauwa: Mfuatano" (2) - Namna ya Kumfahamu Mungu Mwenye Mwili

"Siri ya Utauwa: Mfuatano" (2) - Namna ya Kumfahamu Mungu Mwenye Mwili

Katika siku za mwisho, Mungu amepata mwili kufanya kazi ili kumwokoa mwanadamu. Lakini kwa sababu hatufahamu ukweli wa kupata mwili, tunamchukulia Mungu mwenye mwili kuwa sawa na mwanadamu wa kawaida, hatuwezi kuitambua sauti ya Mungu na tunajua hata kidogo zaidi jinsi ya kumkaribisha Bwana—kufikia kiwango ambacho hata tunaweza kufuata ulimwengu wa dini na nguvu zinazotawala kumkana na kumshutumu Mungu—hali haiwi tofauti na wakati ambapo Mungu alipata mwili kama Bwana Yesu kufanya kazi Yake ya Enzi ya Neema. Kwa hivyo, inaonekana kwamba, kuufahamu ukweli wa kupata mwili ni muhimu sana katika sisi kumjua Mungu. Kwa hiyo kupata mwili ni nini hasa? Ni nini kiini cha kupata mwili?