Jumanne, 6 Machi 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | Unapaswa Kudumisha Ibada Yako Kwa Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Mwenyezi MunguUnapaswa Kudumisha Ibada Yako Kwa Mungu
Mwenyezi Mungu alisema, Roho Mtakatifu Anafanya kazi vipi katika kanisa sasa? Je, una ufahamu wa hilo? Ni matatizo gani makubwa zaidi yanayowakumba ndugu na dada? Wamepungukiwa na nini zaidi? Kwa sasa, kuna watu ambao wako hasi katikati ya majaribio, na wengine wao hata wanalalamika, na wengine hawasongi mbele tena kwa sababu Mungu Hazungumzi tena. Watu hawajaingia njia sahihi ya imani katika Mungu. Hawawezi kuishi wakijitegemea, na hawezi kudumisha maisha yao ya kiroho. Kuna watu wengine ambao wanafuata, wana bidii ya kufuata, na wako tayari kutenda Mungu Akinena. Lakini Mungu Asiponena, hawasongi mbele tena. Watu bado hawajaelewa mapenzi ya Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Wakati Wa Mabadiliko"(2) - Njia ya Pekee ya Kuinuliwa Kwenda Katika Ufalme wa Mbinguni


"Wakati Wa Mabadiliko"(2) - Njia ya Pekee ya Kuinuliwa Kwenda Katika Ufalme wa Mbinguni

Watu wengine huamini, kwa kuwa Mungu aliweza kuumba mbingu na dunia na vitu vyote kwa neno moja, kuweza kuwafufua wafu kwa neno moja, Mungu pia Ataweza kubadili taswira zetu mara moja, kutufanya watakatifu, kutuinua hewani kukutana na Bwana wakati Atakaporudi katika siku za mwisho. Je, kweli ni ili kuinuliwa kwenda katika ufalme wa mbinguni? Je, kazi ya kurudi kwa Mungu katika siku za mwisho rahisi hivyo jinsi tunavyofikiri? Mungu husema, "Lazima ufahamu wala usirahisishe mambo zaidi.

Jumatatu, 5 Machi 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Wakati Wa Mabadiliko"(1) - Wanawali Wenye Hekima Hunyakualiwaje?

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Wakati Wa Mabadiliko"(1) - Wanawali Wenye Hekima Hunyakualiwaje?

Watu wengine huongozwa na maneno ya Paulo katika suala la kumngoja Bwana ili kuinuliwa kwenda katika ufalme wa mbinguni: "Kwa ghafla, kufumba na kufumbua, wakati wa tarumbeta ya mwisho: kwa maana tarumbeta italia, na wafu watafufuliwa bila uovu, na tutabadilishwa" (1Kor 15:52). Wanaamini kwamba ingawa bado tunatenda dhambi siku zote bila kujinasua kutoka kwa pingu za asili ya dhambi, Bwana atazibadili taswira zetu mara moja na kutuleta katika ufalme wa mbinguni Atakapokuja. Pia kuna watu wanaoongozwa na neno la Mungu:

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Ivunje Laana" (6) - Je, Utiifu kwa Wachungaji na Wazee wa Kanisa ni Sawa na Kumtii Mungu?

"Ivunje Laana" (6) - Je, Utiifu kwa Wachungaji na Wazee wa Kanisa ni Sawa na Kumtii Mungu?

Waumini wengine huamini kwamba wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini wamechaguliwa na kuteuliwa na Bwana, na kwamba wote ni watu wanaomtumikia Bwana. Hivyo wanaamini kwamba kuwatii tu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumtii Bwana, na kwamba kuwaasi au kuwahukumu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumpinga Bwana. Wao huamini hata kuwa, katika makanisa, wachungaji na wazee wa kanisa peke ndio huelewa Biblia na huweza kuelezea Biblia, na almradi kile kinachohubiriwa au kufanywa na wachungaji na wazee wa kanisa kinakubaliana na Biblia na kina msingi katika Biblia, basi watu wanapaswa kuwatii na kuwafuata.

Jumapili, 4 Machi 2018

Umeme wa Mashariki | "Ivunje Laana" (5) - Je, Wachungaji na Wazee wa Kanisa wa Ulimwengu wa Dini Wanateuliwa na Bwana Kweli?

Umeme wa Mashariki | "Ivunje Laana" (5) - Je, Wachungaji na Wazee wa Kanisa wa Ulimwengu wa Dini Wanateuliwa na Bwana Kweli?

Mungu mwenyewe hutoa ushuhuda kwa kila mtu Anayemteua na kumtumia. Angalau, wote hupokea uthibitisho wa kazi ya Roho Mtakatifu, huonyesha matunda ya kazi ya Roho Mtakatifu, na wanaweza kuwasaidia watu wa Mungu waliochaguliwa kupokea utoaji wa maisha na uchungaji wa kweli. Kwa sababu Mungu ni mwenye haki na mtakatifu, kila mtu Anayemteua na kumtumia lazima alingane na mapenzi ya Mungu.

"Ivunje Laana" (4) - Je, Imani katika Biblia Ni sawa na Imani katika Bwana?

"Ivunje Laana" (4) - Je, Imani katika Biblia Ni sawa na Imani katika Bwana?

Wachungaji wengi sana na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini huamini kwamba Biblia inamwakilisha Bwana, na kwamba kuamini katika Bwana ni kuamini katika Biblia, na kuamini katika Biblia ni kuamini katika Bwana. Wao huamini kwamba mtu akiachana na Biblia basi hawezi kuitwa muumini, na kwamba mtu anaweza kuokolewa na anaweza kuingia katika ufalme wa mbinguni almradi ashikilie Biblia. Je, Bibilia inaweza kweli kumwakilisha Bwana?