Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Wazee-wa-Kanisa. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Wazee-wa-Kanisa. Onyesha machapisho yote

Jumatatu, 5 Machi 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | "Ivunje Laana" (6) - Je, Utiifu kwa Wachungaji na Wazee wa Kanisa ni Sawa na Kumtii Mungu?

"Ivunje Laana" (6) - Je, Utiifu kwa Wachungaji na Wazee wa Kanisa ni Sawa na Kumtii Mungu?

Waumini wengine huamini kwamba wachungaji na wazee wa kanisa wa ulimwengu wa kidini wamechaguliwa na kuteuliwa na Bwana, na kwamba wote ni watu wanaomtumikia Bwana. Hivyo wanaamini kwamba kuwatii tu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumtii Bwana, na kwamba kuwaasi au kuwahukumu wachungaji na wazee wa kanisa ni kumpinga Bwana. Wao huamini hata kuwa, katika makanisa, wachungaji na wazee wa kanisa peke ndio huelewa Biblia na huweza kuelezea Biblia, na almradi kile kinachohubiriwa au kufanywa na wachungaji na wazee wa kanisa kinakubaliana na Biblia na kina msingi katika Biblia, basi watu wanapaswa kuwatii na kuwafuata.