Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mtu-Mwaminifu. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo Mtu-Mwaminifu. Onyesha machapisho yote

Jumapili, 3 Juni 2018

Kanisa la Mwenyezi Mungu | 61. Si Rahisi Kuwa Mtu Mwaminifu

Zixin    Jiji la Wuhan, Mkoa wa Hubei
Kupitia kula na kunywa neno la Mungu na kusikiliza mahubiri, nilikuja kuelewa umuhimu wa kuwa mtu mwaminifu na hivyo nikaanza kufanya mazoezi kuwa mtu mwaminifu. Baada ya muda, niliona kuwa nilipata kuingia kiasi katika kuwa mtu mwaminifu. Kwa mfano: Wakati wa kuomba au kuzungumza na mtu, ningeweza kuongea ukweli na kutoka kwa moyo; niliweza pia kuchukulia kutekeleza wajibu wangu kwa uzito, na wakati nilipofichua upotovu niliweza kujiweka wazi kwa watu wengine. Kwa sababu ya hili, nilifikiri kuwa mtu mwaminifu lilikuwa jambo rahisi sana kutenda, na sio vigumu hata kidogo kama ilivyodaiwa kuwa na maneno ya Mungu: “Wengi wanaona afadhali washutumiwe hadi kuzimu kuliko kuongea na kutenda kwa uaminifu.” Ni baadaye tu nilipoweza kufahamu kupitia uzoefu kwamba kwa kweli si rahisi kwa mtu mpotovu kuwa mtu mwaminifu. Maneno ya Mungu kwa kweli ni ya kweli kikamilifu na hayajatiwa chumvi kabisa.