Jumanne, 5 Februari 2019

nyimbo za kusifu | 68. Ni Bahati Yetu Nzuri Kumhudumia Mungu

Tunasikia sauti ya Mungu na kuthibitisha kuonekana na kazi ya Mungu.
Tuna bahati sana kukaribisha kurudi kwa Bwana.
Tunahisi msisimko sana kumwona Mungu wa vitendo uso kwa uso.
Ee! Kwa kuhudhuria sikukuu pamoja na Mungu, tunainuliwa hadi katika ufalme wa mbinguni!
Kuanzia sasa kuendelea tutakula, kunywa na kufurahia maneno ya Mungu, tunafurahia sana kuwa na Mungu.
II
Tukitaka sana na kutamani kubarikiwa, tunakutana na ufunuo na hukumu ya maneno ya Mungu.
Mioyo yetu inachomwa na upanga Wake na tunahisi maumivu na uchungu mwingi.
Kwa kumwamini Mungu ili kubarikiwa na kuingia katika ufalme wa mbinguni pekee, wanadamu wapotovu hawastahili kuuona uso wa Mungu.
Ee! Miaka mingi sana ya kutamani imepotea yote, tunadhoofika katika maumivu na mioyo yetu imevunjika.
Maneno ya Mungu yanashinda mioyo yetu, tumeridhika kabisa, na tunaanguka chini mbele Yake.
III
Ni kupitia hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu pekee ndiyo tunaona jinsi ambavyo tumepotoshwa sana.
Tukiwa tumejawa nia na tamaa ya kubarikiwa, tabia zetu potovu hazijatakaswa.
Si tu kwamba hatustahili kuingia katika ufalme wa mbinguni pekee, ila kumhudumia Mungu tayari ni kutukuzwa Kwake.
Ee! Kwa neema ya Mungu ndio tunahudumu, na kuhudumu ni bahati yetu nzuri.
Tuko tayari kumhudumia Mungu kwa uaminifu, na huu ndio upendo na baraka kubwa zaidi ya Mungu.
IV
Leo, tunaweza kumhudumia Mungu, na tunahisi kuwa hatustahili kabisa.
Hatujali ikiwa tutabarikiwa au tutakutana na maafa, wala hatujali hatima yetu itakuwa nini.
Mungu anamshinda Shetani kwa maneno Yake na kutuokoa kutoka gizani.
Ee! Tuko tayari kufanya kazi kama wanyama wa mzigo kwa ajili ya Mungu na kutii mipango na taratibu Zake.
Kwa mioyo yetu yote, tutamhudumia Mungu maisha yetu yote, na tutasifu tabia ya Mungu yenye haki milele.
Kujua zaidi: swahili gospel songs

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni