Jumamosi, 20 Oktoba 2018

Swahili Gospel Video Clip "Mungu Akitoa Sheria"


Swahili Gospel Video Clip "Mungu Akitoa Sheria"
      Baada ya Musa kuwaongoza Waisraeli kutoka Misri, Mungu alitangaza sheria na amri, ambazo ziliyaongoza maisha ya Waisraeli duniani na kuwafundisha watu jinsi ya kumwabudu Mungu. Sheria hizi hazikuwaongoza tu Waisraeli, lakini ziliarifu na kutoa matarajio kwa kuundwa kwa katiba kwa vizazi vijavyo, kuweka msingi kwa mifumo ya kisheria ya wanadamu wa baadaye.

Kabla ya miaka hiyo elfu mbili ambayo Yehova Alifanya kazi Yake, binadamu hakujua chochote na karibu wanadamu wote walizoroteka na kugeuka kuwa waasherati na wapotovu vyote ambavyo vilitangulia mafuriko; mioyo yao haikuwa na nafasi yoyote ya Yehova, wala hata njia Yake. Hawakuwahi kuelewa kazi ambayo Yehova Alikuwa Akienda kufanya; walikosa akili, na hata maarifa, kama vile mitambo inayoishi na kupumua, kutojua binadamu, Mungu, ulimwengu, na maisha vilevile. Ulimwenguni walijihusisha na kupotoka kwingi kama alivyofanya yule nyoka, na kusema mambo mengi ambayo yalimchukiza Yehova, lakini kwa sababu hawakujua lolote, Yehova hakuwaadibu wala kuwafundisha nidhamu. Baada ya mafuriko wakati Nuhu alikuwa na umri wa miaka 601, Yehova Alijionyesha rasmi kwa Nuhu na Akamwongoza yeye na familia yake, Akamwongoza yeye, ndege, na wanyama walionusurika mafuriko na vizazi vyake mpaka mwisho wa Enzi ya Sheria, jumla ya miaka 2,500. Alikuwa rasmi kazini nchini Israeli kwa miaka 2,000, na kipindi ambacho Alikuwa kazini nchini Israeli na nje ya Israeli kilikuwa miaka 500, kwa hivyo kwa pamoja ni miaka 2,500. Kwenye kipindi hiki Aliwaagiza Waisraeli kwamba ili kuweza kumhudumia Yehova, wanafaa kujenga hekalu na kuvalia majoho ya kikuhani, kutembea bila viatu kwenye hekalu wakati wa mapambazuko, na kama wasingefanya hivyo viatu vyao vingechafua hekalu na moto ungetumwa chini kwao kutoka paa la hekalu na kuwateketeza hadi kifo. Walitekeleza wajibu wao na kutii mipango ya Yehova. Walimwomba Yehova hekaluni, na baada ya huhamasishwa na Yehova, yaani baada ya Yehova kuongea, waliwaongoza watu na kuwafunza kwamba wanafaa kumstahi Yehova—Mungu wao. Na Yehova Aliwafunza kwamba wanafaa kulijenga hekalu na madhabahu, na kwa wakati uliotengwa na Yehova, yaani, kwenye msimu wa Pasaka, wanafaa kutayarisha ndama na wanakondoo wachanga kwenye madhabahu kama dhabihu ili kuhudumia Yehova ili kuwazuia wao na kuweza kumstahi Yehova katika mioyo yao. Kama wangetii sheria hii ndicho kingekuwa kipimo cha uaminifu wao kwa Yehova. Yehova pia Aliwatengea siku ya Sabato, siku ya saba ya kuumba Kwake. Siku moja baada ya hiyo, Alifanya siku ya kwanza, siku ya wao kumsifu Yehova, kumpa Yehova dhabihu na kumchezea muziki Yehova. Kwenye siku hii, Yehova Aliwaita makuhani wote kugawanya dhabihu hizo kwenye madhabahu ili watu waweze kula na kufurahia kafara zilizotolewa kwa Yehova. Naye Yehova Akasema kwamba walikuwa wamebarikiwa na walikuwa na sehemu Yake, na kwamba walikuwa ndio watu Wake waliochaguliwa (ambalo ndilo lililokuwa agano la Yehova na wana wa Israeli) Na ndiyo maana, mpaka siku hii watu wa Israeli wangali wanasema kwamba Yehova ndiye Mungu wao pekee na wala si Mungu wa watu wengine.
Kwenye Enzi ya Sheria, Yehova Aliweza kuweka wazi sheria nyingi kwa Musa kupitisha kwa wana wa Israeli waliomfuata kutoka Misri. Yehova Aliwakabidhi sheria hizi wana wa Israeli ambazo hazikuwa na uhusiano wowote na Wamisri, na zilinuiwa kuwazuia wana wa Israeli, na ndiyo yaliyokuwa mahitaji Yake kwao. Kama mtu alitii sheria ya Sabato, kama mtu aliheshimu wazazi wake, kama mtu aliabudu miungu na kadhalika, hizi ndizo zilizokuwa kanuni ambazo mtu alihukumiwa na kujulikana kama mwenye dhambi au mwenye haki. Kama mtu alichomwa na moto wa Yehova, au kupigwa na mawe hadi kufa, au kupokea baraka za Yehova, vyote hivi viliamuliwa kulingana na kama mtu alitii sheria hizi. Wale ambao hawakutilia maanani Sabato wangepigwa mawe hadi kufa. Wale makuhani ambao hawakutilia maanani Sabato wangeteketezwa na moto wa Yehova. Wale ambao hawakuheshimu wazazi wao wangepigwa mawe pia hadi kufa. Haya yote yalishauriwa na Yehova. Yehova Alianzisha sheria Zake na taratibu ili huku Akiyaongoza maisha yao, watu wangeweza kumsikiliza na kuheshimu neno Lake na wala si kuasi neno Lake. Alitumia sheria hizi kuweza kudhibiti kizazi kipya cha binadamu kilichozaliwa, kuweka msingi wa kazi Yake ambayo ingefuata. Na kwa hivyo, sababu ya kazi ambayo Yehova Alifanya, enzi ya kwanza iliitwa Enzi ya Sheria. Ingawaje Yehova Aliongea sana na Alifanya kazi nyingi, Aliwaongoza tu kwa njia nzuri huku Akiwafunza watu hawa wasiojua namna ya kuwa na wema, namna ya kuishi, namna ya kuelewa njia ya Yehova. Katika sehemu kubwa ya kazi Yake kwa hakika Alinuia kuruhusu watu Wake kufuatilia njia Yake na kufuata sheria Yake. Kazi ilifanyiwa watu ambao walikuwa wamepotoka kidogo; haikujali sana mageuzi ya tabia au ukuzi wa maisha. Alijali tu matumizi ya sheria ya kuzuia na kudhibiti watu. Kwa wana wa Israeli wakati huo, Yehova Alikuwa tu Mungu kwenye hekalu, Mungu kwenye mbingu. Alikuwa mnara wa wingu, mnara wa moto. Kile ambacho Yehova Aliwahitaji kufanya kilikuwa ni kutii kile ambacho watu wanajua leo kama sheria na mafundisho Yake—mtu angeweza hata kusema taratibu—kwa sababu kazi ya Yehova haikunuiwa kuwabadilisha, lakini kuwapatia vitu vingi ambavyo binadamu anastahili kuwa navyo, kuwaambia kutoka kwenye kinywa Chake mwenyewe, kwa sababu baada ya binadamu kuumbwa, binadamu hakujua chochote kuhusu kile alichostahili kumiliki. Na kwa hivyo Yehova Aliwapatia vitu walivyostahili kumiliki katika maisha yao hapa ulimwenguni, Akawafanya watu Aliokuwa Amewaongoza kuzidi vizazi vyao, Adamu na Hawa, kwa sababu kile Yehova Alichowapatia kilizidi kile Alichokuwa Amepatia Adamu na Hawa hapo mwanzo. Licha ya hayo yote, kazi ambayo Yehova Alifanya Israeli ilikuwa tu kuongoza binadamu na kuwafanya kumtambua Muumba wao. Hakuwashinda wala kuwabadilisha, Aliwaongoza tu. Hii ndiyo jumla ya kazi ya Yehova kwenye Enzi ya Sheria. Ndiyo maelezo ya ziada, hadithi ya kweli, kiini cha kazi Yake kwenye nchi nzima ya Israeli na mwanzo wa kazi Yake ya miaka elfu sita—katika kudhibiti mwanadamu kwa mkono wa Yehova. Kutokana na haya yote kazi nyingi zaidi ilijitokeza kwenye mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni