Jumamosi, 3 Februari 2018

Sura ya 59. Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

Sura ya 59. Namna ya Kumridhisha Mungu katikati ya Majaribu
Mwenyezi Mungu alisema, Ninaibua maswali machache kwa tafakari yenu: Tangu mara ya mwisho tuliposema kwamba kutakuwa na miaka saba mingine ya majaribu makubwa, iwe ni kwa dhiki au majanga, je, mmegundua kusudi la Mungu kupitia kwa hayo? Ni asili gani ya binadamu mnaweza kuona katika mijibizo na mitazamo ya watu kwa miaka hii saba ya majaribu? Hili litachanganuliwa vipi? Fikirieni hilo. Ninazungumzia asili ya binadamu katika kila ushirika, kufikia chanzo, kuchanganua asili ya binadamu, na kuchanganua kiini.

Sura ya 51. Je Unajua Ukweli Hakika Ni Nini?

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, imani ya kidini

Sura ya 51. Je Unajua Ukweli Hakika Ni Nini?
Mwenyezi Mungu alisema, Ninyi nyote mara nyingi mmepata uzoefu wa hali ya kuwa katika mkutano, na kuhisi kana kwamba huna chochote cha kuhubiri kuhusu—hatimaye unajilazimisha na unasema kitu cha juu juu. Unajua vizuri kuwa maneno haya ya juu juu ni kanuni, lakini unahubiri kuyahusu hata hivyo, na mwishowe unahisi kuwa huna shauku, na watu chini yako wanasikiliza na wanahisi kuwa yanachosha sana—je hilo halijafanyika?

Ijumaa, 2 Februari 2018

Sura ya 28. Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

Sura ya 28. Bila Ukweli Ni Rahisi Kumkosea Mungu

Mwenyezi Mungu alisema, Kutoa kwenu "muhtasari kuhusu ukweli" hakufanywi ili kuwawezesha watu kupata maisha au kupata mabadiliko katika tabia zao kutoka kwa ukweli. Badala yake, kunafanywa ili watu waweze kuwa weledi wa maarifa na mafundisho fulani kutoka kwa ukweli. Wao huonekana kana kwamba wanaelewa lengo lililokusudiwa katika kazi ya Mungu, wakati kwa kweli wamekuwa weledi wa baadhi ya maneno ya mafundisho tu. Hawaelewi maana iliyokusudiwa ya ukweli, na si tofauti na kusomea theolojia au kusoma Biblia.

Umeme wa Mashariki | Sura ya 15. Kutoka katika Siasa Isiyo na Kadri hadi Kutafuta kuwa Msaliaji

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki, Kanisa

1. Uhamaji wa Watu kuelekea kwenye Siasa Isiyo na Kadri
Je, nyote mmekuwa mkitafuta nini hivi karibuni? Je, imekuwa mabadiliko ya tabia na kuwa na ushuhuda wa Mungu? Haijakuwa hiyo! Nawaona watu wengi tena wakitafuta kufa kwa ajili ya Mungu ili kumuaibisha Shetani. Je, mnasubiri tu kuadhibiwa badala ya kupanga kutenda ukweli ama kutafuta kubadilishwa kwa tabia, kulipiza upendo wa Mungu? Baada ya kusoma “Usaliti (1) “na “Usaliti (2), “watu walikuwa na mipango ya kufa.

Alhamisi, 1 Februari 2018

Swahili Gospel Video "Kanisa la Nafsi Tatu ni Mwavuli Wangu"

Wakati mmoja, serikali ya Kikomunisti ya Uchina iliwakamata Wakristo wengi wa Kanisa la Mwenyezi Mungu kutoka mahali fulani usiku wa manane. Jambo hili lilisababisha ghasia kubwa mahali hapo. Lilichochea majadiliano miongoni mwa washirika wa Kanisa la Nafsi Tatu. Watu wengine waliamini kwamba Umeme wa Mashariki umepitia ukandamizaji na mateso ya kikatili ya serikali ya kikomunisti ya Uchina.

Ushuhuda wa Kuipitia Hukumu ya Kristo | 75. Hatimaye Naishi kwa Kudhihirisha Kiasi Kama Mwanadamu

Kanisa la Mwenyezi Mungu, Umeme wa Mashariki

75. Hatimaye Naishi kwa Kudhihirisha Kiasi Kama Mwanadamu
Xiangwang Mkoa wa Sichuan
Ninahisi kuadibiwa sana moyoni mwangu kila mara ninapoona kwamba maneno ya Mungu yanasema: “Wanadamu dhalimu, wakatili! Kufumba macho na kula njama, kusukumana, kung’ang’ania sifa na mali, kuuana—haya yote yataisha lini? Mungu amezungumza maelfu na mamia ya maneno, ilhali hakuna hata mmoja ambaye amejifahamu. Wanatenda matendo kwa ajili ya familia zao na watoto wao, kazi zao, matarajio, hali katika jamii, majivuno na pesa, kwa sababu ya nguo, kwa sababu ya chakula na mwili—matendo ya nani kwa kweli ni kwa ajili ya Mungu? Hata miongoni mwa wale ambao matendo yao ni kwa ajili ya Mungu, ni wachache tu wanaomfahamu Mungu.