38. Siri Niliyoishikilia kwa Kina Ndani ya Moyo Wangu
Wuzhi Mji wa Linyi, Mkoa wa Shandong
Katika majira ya kuchipua ya mwaka wa 2006, nilinyang'anywa cheo changu kama kiongozi na nikarudishwa nilikotoka kwa sababu nilifikiriwa kuwa "bwana ndiyo" sana. Niliporejea mara ya kwanza, nilitumbukia ndani ya kikalibu cha mateso na maumivu makubwa. Sikuwahi kufikiri kwamba baada ya miaka mingi ya uongozi mambo yangeharibika kwa sababu ya kuwa "bwana ndiyo." Huu ulikuwa ndio mwisho kwangu, nilidhani, kila mtu aliyenijua angejua juu ya kushindwa kwangu na ningefanywa kama mfano mbaya katika kanisa. Ningewezaje kukabiliana na wengine baada ya haya yote? Jinsi nilivyozidi kufikiria, ndivyo nilivyozidi kuwa hasi, mpaka hatimaye nikapoteza imani ya kuendelea kutafuta ukweli. Hata hivyo, wakati nilifikiri juu ya sadaka zote na matumizi niliyoyatoa katika miaka hii michache iliyopita,